Photobucket

Tuesday, March 27, 2012

Rose Muhando kufanya shoo kwa ajili ya kusaidia yatima

Mwanamuziki wa nyimbo za  Injili nchini Dada Rose Muhando anayetamba kwa kibao chake 'Utamu wa Yesu',ameeleza kuwa ana mpango wakufanya shoo kubwa siku ya pasaka tarehe 8 ya mwezi wa nne eneo la uwanja wa Taifa.Vilevile alieleza kuwa kuna baadhi ya wasanii kutoka nje ya nchi ambao watakuja kushirikiana naye kwenye shoo hiyo mmoja wapo ni Rebecca Malope kutoka Afrika ya Kusini ambaye yupo tayari kabisa kuja kushiriki.
Aidha Mkurugenzi wa Msama Promotion Bwana Alex Msama alieleza kuwa Mh.Bernard Membe waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa atakuwa Mgeni rasmi.Wengine ni wakuu mbalimali wa serikali,wafanya biashara na wengine wengi.
Rose Muhando anatarajia kushirikiana na wasanii mbali mbali wa muziki Maryanne Tutuma na Anastazia Mukubwa wa Kenya.Kwa upande wa Tanzania ni Christina Shusho,Upendo Nkone,Upendo Kilahilo,Atosha Kissava,Ephraim Sekeleti,Glorious Celebration Group,Kinindoni Revival Choir na vile vile Faraja Ntaboba kutoka Jamuhuli ya Kidemokrasia ya Kongo
"Kuna wasanii wengi ambao wamekubali kuungana kushiriki kwenye hiyo shoo"Alieleza Msama
Kiingilio itakuwa 2000/- kwa mtoto,5000/- kwa wakubwa na 10,000/- kwa viti maalumu

No comments:

Post a Comment