Jumamosi ya April 14 2012 kutakuwa na mechi ya kirafiki kati ya Wasanii wa filamu Bongo Movie.Lengo la mechi hiyo ni kuchangia Twiga Stars,timu hiyo ya wanawake iliyo katika mchujo wa Kombe la Afrika la wanawake(AWC).Michuano hiyo itafanyika nchini Equatorial Guinea mwezi Novemba ya mwaka huu.
Aidha asilimia mbili ya kitakachopatikana kwenye mechi kiyo ya kirafiki itapelekwa kwenye familia ya aliyekuwa msanii wa filamu Nje na Ndani ya Tanzania Marehemu Steven Kanumba.
Kiingilio kitakuwa 10,000 kwa VIP A, 5,000 kwa VIP B na C na 2000 kwa viti vya rangi ya kijani,blue na chungwa
Mechi itaanza mishale ya saa 10 jioni..
Wote mnakaribishwa.
RAIS DKT SAMIA ATUMA UJUMBE MAALUM KWA RAIS WA CHINA
-
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan
akimkabidhi Waziri wa Idara ya Kimataifa ya Chama cha Kikomunisti cha China
Mhe. ...
6 hours ago




No comments:
Post a Comment