Matatizo yanayoikumba sekta ya Elimu
Matatizo yanayoikumba sekta ya elimu yameonekana kama ni ishara mbaya kwa nchi huko mbeleni kama hayatashughulikiwa.Hayo yamesemwa na mratibu wa Tanzania Education Network(TEN) Helima Mangele katika mkutano wa tano wa elimu bora uliofanyika Dar Es Salaam
Alisema kuna changamoto mbalimbali zinazokabili sekta hiyo ya Elimu ikiwemo uchache wa walimu,vitendea kazi pamoja na miundo mbinu.Aidha alieleza kuwa serikali inadhamira ya kukuza elimu kwa kuongeza shule ambayo hiyo itasaidia kuongeza elimu ya sekondari kwa wananchi.Alisema serikali imefanikiwa kufanya hivyo lakini bado kuna changamoto zinazoikabili sekta hiyo kama ukosefu wa walimu na miundombinu
STANBIC YAHIMIZA UFADHILI UNAONGOZWA NA WAAFRIKA ILI KUFUNGUA FURSA ZA
MIUNDOMBINU BARANI AFRIKA
-
Afrika inapaswa kutumia zaidi mitaji yake ya ndani, kuimarisha ushirikiano
wa kikanda na kukuza masoko ya fedha ya ndani ili kuziba pengo la ufadhili
wa ...
7 hours ago



No comments:
Post a Comment